Baraka

Picha takatifu ya Yesu Kristo Pantokrator iliyochorwa na Theofane Mgiriki (karne ya 14). Mkono wake wa kulia umeinuliwa ili kubariki.

Baraka ni tendo la kumtakia au kumuombea mtu mema, hasa kutoka kwa Mungu. Pengine mtendaji ana mamlaka fulani juu ya yule anayeombewa (kwa mfano ni mzazi), hasa katika dini husika (kwa mfano ni kuhani).

Baraka zinaweza kulenga maisha ya kawaida (afya, uhai, uzazi, amani, mafanikio n.k.) au mema ya kiroho zaidi (utakaso).


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne