Dini

Nembo za Kidini:
1.: Ukristo - Uyahudi - Uhindu - Nyota ya Baha'i
2.: Uislamu - Msalaba wa Kikelti - Falsafa ya China-Korea - Shinto
3.: Ubuddha - Usikhi - Ujaini - Ujaini
4.: Ayyavali - Upagani mpya - Msalaba wa chuma - Msalaba wa Kislavoni
Mganga wa kienyeji, Peru, 1988.

Dini (kutoka Kiarabu اﻟدﻴن, tamka: ad-din) inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji.

Ibada ni nguzo mojawapo iliyo dhahiri miongoni mwa dini kadhaa katika kuunganisha dhamira za mwenye kushika dini na mhimili wa imani, lakini dini inahusu pia mafundisho kuhusu maadili, mema na mabaya, imani na jinsi ya kushiriki katika jumuiya za waumini.

Kwa maana nyingine "dini" inataja jina kielelezo juu ya aina mbalimbali za imani jinsi inavyopatikana duniani, yaani jumuiya za kidini.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne