Fizikia

Sumaku ikielea juu ya kipitishiumeme kikuu kuonyesha Ifekti ya Meissner.

Fizikia (kutoka neno la Kigiriki φυσικός, physikos, "ya kimaumbile", ambalo tena linatokana na φύσις, physis, "umbile") ni fani ya sayansi inayohusu maumbile ya ulimwengu, hususan asili ya dunia na viumbe vyote.

Ni taaluma yenye kushughulika na maada na uhusiano wake na nishati.

Fizikia imetoa mchango mkubwa katika sayansi, teknolojia na falsafa.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne