Haki

Maadili bawaba
Haki.
Haki ilivyoonyeshwa na Luca Giordano.
Bibi Haki, kielelezo cha adili hili, amechorwa kama mungu wa kike akiwa na vifaa vitatu: upanga, mizani na kitambaa machoni.[1]

Haki (kwa Kiingereza: justice, kutoka neno la Kilatini: justitia ambalo mzizi wake ni jus, haki, unaopatikana katika justus, mwenye kujali haki) ndiyo utaratibu unaotakiwa katika mafungamano yoyote kwa kuwa ni adili la msingi la utu linalotufanya tumpatie mwingine anachostahili..

Kwa Kigiriki inaitwa dikaiosyne, kutokana na neno asili dike yaani anayeelekeza na kwa hiyo pia mwongozo, utaratibu. Tofauti na nomos, yaani sheria inayoongoza wanyama pia, dike inahitajiwa na binadamu ili kuishi kwa utaratibu. Ni kinyume cha bie, ukatili, nguvu inayoangamiza. Dikaios (mwenye kujali haki), ni mtu anayemtendea kila mmoja haki yake. Dikaia zoe ni maisha ya kiutu yanayopingana na hybris (kiburi) na ushenzi.

Maana ya haki inatofautiana kwa kila utamaduni. Katika maana ya kwanza kabisa ambayo ilitafsiriwa na mwanafalsafa wa Ugiriki, Plato kwenye kazi yake Jamhuri[2]. Kutokana na historia dhana mbalimbali zimegunduliwa.

  1. Luban, Law's Blindfold, 23.
  2. Plato, Republic trans. Robin Waterfield (Oxford: Oxford University Press, 1984).

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne