Jangwa

Matuta ya mchanga katika Sahara ya Libya
Nguzo za mwamba katika Jangwa la Australia
Jangwa la Atacama

Jangwa ni eneo kavu lenye mvua au usimbishaji kidogo tu. Kutokana na ukavu kuna mimea michache tu, pia wanyama wachache. Wanyama walioko hufanya shughuli zao hasa wakati wa usiku. Kipimo cha usimbishaji kinachotambulika kimataifa ni kiwango cha chini ya mm 250 kwa mwaka[1]. Uoto wa mimea hufunika chini ya asilimia 5 za eneo lake.

Wakati mwingine huitwa jangwa hata maeneo ambayo ni makavu kutokana na baridi kali.

  1. Marshak (2009). Essentials of Geology, 3rd ed. W. W. Norton & Co. p. 452. ISBN 978-0-393-19656-6.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne