Johannes Gutenberg

Johannes Gutenberg
Biblia iliyochapwa na Gutenberg mwaka 1455 hivi.
Wachapishaji wa karne ya 16

Johannes Gensfleisch zur Laden zum Gutenberg, anayejulikana kifupi kama Johannes Gutenberg, (mnamo 1398 - 3 Februari 1468) alikuwa fundi dhahabu na mvumbuzi kutoka Ujerumani anayekumbukwa hasa kama mbuni wa uchapaji vitabu kwa herufi za kusogezeka.

Alitengeneza mashine ya kwanza ya kuchapa vitabu, alibuni aloi ya kufaa kwa herufi alizotumia katika mashine hii pamoja na wino.

Alitengeneza pia kifaa kilichomwezesha kusubu herufi za metali haraka.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne