Kalenda ya Gregori | 2024 MMXXIV |
Kalenda ya Kiyahudi | 5784 – 5785 |
Ab urbe condita (Roma ya Kale) | 2777 |
Kalenda ya Ethiopia | 2016 – 2017 |
Kalenda ya Kiarmenia | 1473 ԹՎ ՌՆՀԳ |
Kalenda ya Kiislamu | 1446 – 1447 |
Kalenda ya Kiajemi | 1402 – 1403 |
Kalenda za Kihindu | |
- Vikram Samvat | 2079 – 2080 |
- Shaka Samvat | 1946 – 1947 |
- Kali Yuga | 5125 – 5126 |
Kalenda ya Kichina | 4720 – 4721 癸卯 – 甲辰 |
Kalenda ni utaratibu wa kupanga wakati. Hupatikana kama orodha ya vipindi vya wakati kama vile siku, juma, mwezi na mwaka. Kalenda mbalimbali zimejua pia vipindi vya miaka kadhaa.
Kalenda inayotumika zaidi leo kimataifa ni kalenda ya Gregori iliyo muhimu kwa uchumi na biashara. Kuna pia nchi zinazotumia hasa kalenda zao za kitaifa au kalenda mbalimbali sambamba.
Hasa maisha ya kidini hupangwa kufuatana na kalenda maalumu. Kihistoria palikuwako na kalenda nyingi.