Kanuni ya Biblia

Gombo la Abisha ni la zamani kuliko yote ya Torati waliyonayo Wasamaria na labda kuliko yote yaliyoko duniani; linapatikana Nablus.

Kanuni ya Biblia ndiyo orodha rasmi ya vitabu vitakatifu vya Biblia kadiri ya dini au madhehebu fulani.[1]

Neno "kanuni" limeenea kutokana na lile la Kigiriki "κανών", ambalo asili yake ni ya Kiashuru na lina maana ya "kipimo".[2]

Kwa mfano, Wasamaria wanakubali vitabu vitano vya Torati tu, tofauti na Wayahudi ambao katika Biblia ya Kiebrania (Tanakh) wanakubali pia vitabu vya Manabii wa awali na Manabii wa baadaye pamoja na vitatu vingine, hasa Zaburi.

Upande wa Ukristo, Wakatoliki wanavyo 73 katika Agano la Kale na Agano Jipya, wakati Waprotestanti wanavyo 66 tu. Tofauti hiyo katika matoleo ya Biblia ya Kikristo inaitwa suala la Deuterokanoni.

  1. McDonald, L. M. & Sanders, J. A., eds. (2002). The Canon Debate. "The Notion and Definition of Canon." pp. 29, 34. (In the article written by Eugene Ulrich, "canon" is defined as follows: "...the definitive list of inspired, authoritative books which constitute the recognized and accepted body of sacred scripture of a major religious group, that definitive list being the result of inclusive and exclusive decisions after serious deliberation." It is further defined as follows: "...the definitive, closed list of the books that constitute the authentic contents of scripture.")
  2. McDonald & Sanders, editors of The Canon Debate, 2002, The Notion and Definition of Canon by Eugene Ulrich, page 28: "The term is late and Christian ... though the idea is Jewish"; also from the Introduction on page 13: "We should be clear, however, that the current use of the term "canon" to refer to a collection of scripture books was introduced by David Ruhnken in 1768 in his Historia critica oratorum graecorum for lists of sacred scriptures. While it is tempting to think that such usage has its origins in antiquity in reference to a closed collection of scriptures, such is not the case." The technical discussion includes Athanasius's use of "kanonizomenon=canonized" and Eusebius's use of kanon and "endiathekous biblous=encovenanted books" and the Mishnaic term Sefarim Hizonim (external books).

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne