Kiambishi

Kiambishi ni kipande cha neno chenye maana ya kisarufi ambacho kinapachikwa kwa mfano kabla au baada ya mzizi wa neno katika vitenzi na kuwakilisha dhana fulani. [1]

Miongoni mwa viambishi vya Kiswahili mna NI, NDI, KI, KA na kadhalika.

Kiambishi kikitangulia mzizi au kiini cha neno kinaitwa kiambishi awali, kikifuata kinaitwa kiambishi tamati.

  1. * Masuko Christopher Saluhaya, 2013. ISBN 978 9987 9581 1 5.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne