Malaika

Malaika wa uhuru.
Malaika aliyejeruhiwa, mchoro wa Hugo Simberg, 1903.

Malaika katika imani ya dini mbalimbali, kama vile Uyahudi, Ukristo na Uislamu, ni kiumbe wa kiroho tu anayeweza kutumwa na Mungu kwa binadamu.

Kwa umbile lake hawezi kujulikana na hisi za mwili wetu.

Katika Biblia hawa tu wanatajwa kwa jina maalumu: malaika Mikaeli, malaika Gabrieli na malaika Rafaeli (huyo katika Deuterokanoni tu).

Katika Uislamu ni kiumbe chepesi ambacho kimeumbwa kwa nuru, nacho huwa hakanyagi chini kama mwanadamu, bali huelea juu au kuketi ndani ya moyo wa mwanadamu.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne