Mfalme

Aina za serikali duniani
aina za Jamhuri: buluu, kijani, njano na machungwa;
Ufalme:
nyekundu Ufalme wa kikatiba ambapo mfalme ana madaraka madogo tu ya kisiasa
zambarau:Ufalme wa kikatiba ambapo mfalme ana madaraka makubwa
dhambarau nyeusi: mfalme ana madaraka yote asibanwe na katiba
Mengine: Utawala wa chama kimoja au kamati ya kijeshi

Mfalme ni mtawala wa kiume juu ya nchi katika utaratibu wa ufalme. Kwa kawaida amerithi cheo chake kutoka kwa mzazi wake aliyekuwa mfalme pia. Lakini kuna pia wafalme waliochaguliwa au kuteuliwa kwa namna nyingine, hasa kama mfalme aliyetangulia alikufa bila kuacha mrithi.

Utawala wa kifalme ulikuwa wa kawaida katika nchi nyingi za dunia kwa muda mrefu.

Mwanamke anayeshika nafasi ya mfalme huitwa "malkia".

Kama cheo kinaendelea katika ukoo mmoja kutoka mababa kwa watoto wao familia hiyo huitwa nasaba.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne