Mkoa wa Dodoma

Dodoma
Mahali pa Mkoa wa Dodoma katika Tanzania
Mkoa wa Dodoma

Mkoa wa Dodoma ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 41000[1]. Uko katikati ya nchi na umepakana na mikoa ya Manyara, Morogoro, Iringa na Singida.

Eneo lote la mkoa lina km² 41,310. Sehemu kubwa ni nyanda za juu kati ya mita 830 hadi 2000 juu ya UB.

Katika sensa ya mwaka 2022, idadi ya wakazi wa Mkoa wa Dodoma ilihesabiwa kuwa 3,085,625. [2]

Kuna wilaya nane zifuatazo: Bahi, Chamwino, Chemba, Dodoma Mjini, Kondoa, Kondoa Mjini, Kongwa, Mpwapwa. Wilaya ya awali ya Dodoma Vijijini imegawiwa katika wilaya mpya za Chamwino na Bahi. Mnamo Machi 2012 ilianzishwa wilaya mpya ya Chemba. Pia Wilaya ya Kondoa imegawiwa sehemu mbili.

  1. "Nakala iliyohifadhiwa" (PDF). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 2020-03-21. Iliwekwa mnamo 2017-09-23.
  2. https://www.nbs.go.tz

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne