Mwili wa Kristo

Uanzishwaji wa Ekaristi, mchoro wa Nicolas Poussin, 1640.


Mwili wa Kristo ni namna ambayo Mtume Paulo na wengineo walichambua fumbo la Kanisa kama umoja wa waamini wote, ukiwa na Yesu kama kichwa chake[1]. Ndiye anayesadikiwa kuwa chemchemi ya ukombozi wa wanadamu wote pale alipolifia Kanisa na kuliachia sakramenti kuu ya Pasaka, yaani ekaristi takatifu.

Utakatifu wetu unategemea nguvu zinazomtoka mfululizo Kristo Mkombozi ambaye, kwa njia ya sakramenti na hata nje ya hizo, anatushirikisha neema alizotustahilia alipoishi duniani, kwa namna ya pekee wakati wa mateso yake.

  1. Mystici corporis Christi, a papal encyclical issued by Pope Pius XII, sections 60–62

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne