Sala

Yesu akisali katika mateso yake huko Gethsemane kadiri ya Heinrich Hofmann.
Mwanamume Mshinto wa Japani akisali peke yake.
Wanawake Wakristo wa Urusi wakisali pamoja.

Sala (kutoka neno la Kiarabu صلاة‎, ṣalāh; pia maombi) ni njia ambayo binadamu anauelekea ulimwengu wa roho, hasa kwa nia ya kuongea na Mungu kwa sauti au kimoyomoyo.

Malengo yake yanaweza kuwa tofauti: kusifu, kushukuru, kuomba au kujiachilia.

Upande wa pili sala ni kutafakari ili kusikiliza na kuelewa ujumbe wa Mungu.

Sala inaweza kufanywa na mtu peke yake au na wengi pamoja, hata kwa kuimba.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne