Sensa

Sensa za mwisho duniani kote (2013).

Sensa ni utaratibu wa kupata na kutunza habari kuhusu idadi ya watu, makazi au taasisi fulanifulani katika nchi husika. Pia ni utaratibu rasmi wa mara kwa mara wa kuhesabu idadi ya watu hao.[1] [2]

Sensa hutofautiana na njia ya sampuli ambapo habari zinapatikana kutoka sehemu ndogo tu ya idadi ya watu, wakati mwingine kama makisio ya kisensa. Takwimu za sensa kwa kawaida hutumiwa kwa utafiti, biashara ya masoko, na mipango kama njia bora kwa msingi wa utafiti wa sampuli. Katika baadhi ya nchi, takwimu za sensa hutumiwa kwa kugawanya uwakilishi katika bunge la taifa (wakati mwingine kiutata - tazama mfano Utah v. Evans).

Inatambulika sana kwamba idadi ya watu na makazi ni muhimu kwa ajili ya mipango ya jamii yoyote. Njia za jadi za sensa, hata hivyo, zimekuwa ghali zaidi.

  1. Shepard, Jon (2003). Sociology and You. Ohio: Glencoe McGraw-Hill. ku. A-22. ISBN 0078285763. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2010-03-08. Iliwekwa mnamo 2009-12-14. {{cite book}}: Unknown parameter |coauthors= ignored (|author= suggested) (help); Unknown parameter |dead-url= ignored (|url-status= suggested) (help)
  2. Sullivan, Arthur (2003). Economics: Principles in action. Upper Saddle River, New Jersey 07458: Prentice Hall. uk. 334. ISBN 0-13-063085-3. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-12-20. Iliwekwa mnamo 2021-02-24. {{cite book}}: Unknown parameter |coauthors= ignored (|author= suggested) (help); Unknown parameter |dead-url= ignored (|url-status= suggested) (help)CS1 maint: location (link)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne