Sintaksi

Sintaksi (au sarufi miundo/muundo) ni tawi la isimu au taaluma ya sarufi inayoshughulikia namna ambavyo vikundi vya maneno na sentensi mbalimbali zinajengwa katika lugha. Hasa hushughulikia kanuni zinazotawala mfumo wa vipashio vya lugha. Sarufi muundo hushughulikia kanuni zinazotawala mpangilio wa maneno katika lugha husika ili kujenga (kuunda tungo yenye maana). Kipashio ni kipande cha neno au kikundi cha maneno yanayotoa taarifa fulani katika lugha ya Kiswahili. Kuna vipashio vitano - navyo ni: Mofimu --> Neno --> --> Kirai --> Kishazi --> Sentensi. Katika namna ya kutaja au kutumia vipashio, ngazi ya mofimu ni ndogo kuliko neno. Neno ni ndogo kuliko Kirai. Kirai ni kidogo kuliko Kishazi. Kishazi ni kidogo kuliko Sentensi. Hivyo basi mpangilio wake halisi huanza kwa ukubwa na kuja udogo.

Mfano, ukubwa kwenda udogo:

5. Sentensi

4. Kishazi

3. Kirai

2. Neno

1. Mofimu

Taaluma nyingine za sarufi ni pamoja na fonolojia, mofolojia au semantiki.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne