Sita

Mabadiliko katika kuandika sita.

Sita ni namba ambayo inafuata tano na kutangulia saba. Kwa kawaida inaandikwa 6 lakini VI kwa namba za Kiroma na ٦ kwa zile za Kiarabu.

Vigawo vyake vya namba tasa ni: 2 x 3.

Namba hiyo katika Kiswahili ina asili ya Kiarabu pamoja na sitini (sita mara kumi).


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne