Tahajia

Tahajia (kutoka neno la Kiarabu; pia othografia au orthografia kutoka neno la Kiingereza orthography ambalo lina asili ya Kigiriki) ni utaratibu wa kuandika maneno kwa namna inayokubalika kwa mujibu wa sheria, kanuni na mapatano ya lugha husika. Kila lugha huwa na kanuni na mapatano kuhusu jinsi ya kuandika maneno.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne