Uchapaji

Matbaa ya karne ya 15: Fundi anakaza karatasi, wengi hutazama kurasa zilizochapwa tayari

Uchapaji ni njia ya kunakili maandishi na picha kwa karatasi au loho bapa nyingine, hata kitambaa.

Vitabu na magazeti vinatengenezwa kwa njia ya uchapaji. Hivyo vinaweza kutolewa kirahisi kwa nakala nyingi.

Kabla ya kupatikana kwa uchapaji vitabu, hati na maandiko yote yalinakiliwa kwa mkono pekee. Katika tamaduni mbalimbali waandishi na wanakili walikuwa mabingwa muhimu. Lakini kunakili matini ndefu kama kitabu kulichukua muda mrefu, hata miaka, hivyo vitabu havikupatikana kwa nakala nyingi, pia vilikuwa ghali mno.

Tangu kubuniwa kwa uchapaji maandishi yamepatikana kwa wingi tena kwa bei nafuu. Hii ilisaidia uenezaji wa habari na elimu na kusababisha mapinduzi makuu katika historia ya binadamu.[1][2][3][4]

  1. Robinson. Andrew 1995. The story of writing. Thames & Hudson, London.
  2. Christin, Anne-Marie (ed) A history of writing. Flammarion, Paris.
  3. Gaur, Albertine 1992. A history of writing. 3rd ed.
  4. Diringer, David 1968. The alphabet: a key to the history of mankind.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne