Ufunguo

Ufunguo wa Waviking wa Uingereza (900 hivi BK)
Kufuli za karne za kati huko Kathmandu (Nepal).

Ufunguo (kutoka kitenzi "kufunga", kinyume chake "kufungua") ni kifaa kinachotumika kufungulia au kufungia mlango, kufuli n.k.

Kwa sababu hiyo, mara nyingi huchukuliwa kama ishara ya kumiliki nyumba, sanduku n.k. Mwambatanisho wa kufuli na ufunguo huchangia katika ulinzi kwa maana ni mwenye ufunguo peke yake anayeweza kufungua kitasa au kufuli.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne