Uinjilishaji


Uinjilishaji (kutoka neno Injili) ni msamiati wa teolojia ya Kikristo ambao unajumlisha kazi mbili tofauti: kutangaza Injili kwa wasio Wakristo ili wamuamini Yesu Kristo[1], na kurekebisha jamii nzima ili isiishi kinyume na maadili yanayodaiwa na Mungu bali imani ipenye utamaduni wa waumini na kwa njia yao ule wa umati[2]. Ndiyo sababu hauishii katika kutangaza mbiu ya kwanza bali inaendelea katika katekesi na malezi kwa jumla, kwa mfano katika shule za Kanisa.

  1. Timothy J. Demy Ph.D., Paul R. Shockley Ph.D., Evangelical America: An Encyclopedia of Contemporary American Religious Culture, ABC-CLIO, USA, 2017, p. 466
  2. Exhortación apostólica Evangelii Nuntiandi, Pablo VI

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne