Ukombozi

"Kuvuka Bahari ya Shamu" kadiri ya Nicholas Poussin. Tukio hilo la karne ya 13 KK ndilo ukombozi wa msingi kwa taifa la Israeli.

Ukombozi, katika dini nyingi, ni msamaha au ondoleo la dhambi zilizopita na kinga dhidi ya laana na mateso mbalimbali, ya milele au ya muda.

Kwa kawaida ukombozi unasadikiwa kupatikana kwa njia ya kafara au sadaka fulani.

Kati ya dini zinazofundisha ukombozi, kuna Uhindu, Ubuddha na dini za Abrahamu, hasa Ukristo na Uislamu.

Katika aina kadhaa ya Ubuddha, ukombozi unaweza ukapatikana kwa juhudi za mhusika, anapofaulu kubandukana na tamaa zote.[1]

Katika Uyahudi, ukombozi ni ule ambao Mungu aliwatoa Wanaisraeli kutoka Misri, halafu kutoka Mesopotamia.[2]

Katika teolojia ya Ukristo, ukombozi ni hasa ule uliofanywa na Yesu kwa kulipia dhambi za wote msalabani halafu kufufuka mtukufu.[3][4]Waamini wanashiriki kiibada tukio hilo kwa njia ya ubatizo kwanza, na kwa kushiriki ekaristi maisha yao yote.

Katika Uislamu, ukombozi unafikiwa kwa kutofanya tendo lolote lisilolingana na dini hiyo.[5][6] Muislamu akifanya dhambi anatakiwa kumrudia Mungu kwa toba na matendo mema, kama sala na sadaka.[7][8][9]

  1. Spiro, Melford (1982). Buddhism and Society: A Great Tradition and Its Burmese Vicissitudes. ku. xiv.
  2. "Reb on the Web". Kolel: The Adult Centre for Liberal Jewish Learning. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-07-21. Iliwekwa mnamo Novemba 1, 2010.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. Morris, Leon (1962). Redeemer, Redemption, 'The New Bible Dictionary'. Grand Rapids: William B. Eerdmans Publishing Company. ku. 1078–1079.
  4. "Redemption." Christian Classics Ethereal Library at Calvin College. July 2, 2009. http://www.ccel.org/s/schaff/encyc/encyc09/htm/iv.vii.lxxxv.htm
  5. Hava Lazarus-Yafeh (1981). Some Religious Aspects of Islam: A Collection of Articles. Brill Archive. uk. 48. ISBN 9789004063297. Iliwekwa mnamo 18 Februari 2015.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  6. Yahiya Emerick (1 Nov 2011). The Complete Idiot's Guide to Islam, 3rd Edition. Penguin. ISBN 9781101558812. Salvation and redemption: Islam says our sincere faith and virtuous actions get us into heaven, not just a one-time conversion moment. {{cite book}}: |access-date= requires |url= (help)CS1 maint: date auto-translated (link)
  7. Mahmoud Mustafa Ayoub. "The Idea of Redemption in Christianity and Islam". BYU. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-07-13. Iliwekwa mnamo 18 Februari 2015.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  8. Chawkat Georges Moucarry (2001). Faith to Faith: Christianity & Islam in Dialogue. Inter-Varsity Press. uk. 110. ISBN 9780851118994. {{cite book}}: |access-date= requires |url= (help)CS1 maint: date auto-translated (link)
  9. Hava Lazarus-Yafeh (1981). Some Religious Aspects of Islam: A Collection of Articles. Brill Archive. uk. 48. ISBN 9789004063297. Iliwekwa mnamo 18 Februari 2015.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne