Wilaya ya Sengerema

Mahali pa Sengerema (kijani cheusi) katika mkoa wa Mwanza kabla haujamegwa.

Wilaya ya Sengerema ni wilaya mojawapo kati ya 8 za Mkoa wa Mwanza yenye postikodi namba 33300.

Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 663,034 waishio humo. [1] na katika ile ya mwaka 2022 walihesabiwa 425,415 [2].

Makao makuu ya wilaya yako kwenye mji wa Sengerema wenye kata nne za Ibisabageni, Mwabaluhi (Mwambului), Nyampulukano na Nyatukala.

Misimbo ya posta katika wilaya hii inaanza na tarakimu 333.

Kuna Telecentre Wilayani Sengerema. Ipo kwenye kwenye makutano ya barabara za Kamanga na Busisi.

  1. Sensa ya 2012, Mwanza Region - Sengerema District Council
  2. https://www.nbs.go.tz

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne