Jamhuri ya Angola República de Angola (Kireno) | |
---|---|
Kaulimbiu: Virtus Unita Fortior (Kilatini) "Maadili ni ya nguvu zaidi yakiungana" | |
Wimbo wa taifa: Angola Avante "Nenda mbele, Angola" | |
Mji mkuu na mkubwa | Luanda |
Lugha rasmi | Kireno |
Lugha za taifa | Chokwe, Kimbundu, Kikongo, Oshiwambo, Luchazi, Umbundu |
Kabila (2021) |
|
Dini (2019) |
|
• Rais | João Lourenço |
• Naibu rais | Esperança da Costa |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2023 | 35 981 281[1] |
HDI (2022) | ![]() kati (ya 150) |
Sarafu | Kwanza ya Angola |
Majira ya saa | UTC+1 (WAT) |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +244 |
Jina la kikoa | .ao |
Angola ni nchi kubwa iliyopo upande wa kusini magharibi wa bara la Afrika ikipakana na Namibia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Zambia. Upande wa magharibi kuna pwani ndefu ya Bahari Atlantiki. Mkoa wa Kabinda umetenganika na sehemu nyingine za nchi na unapakana na Jamhuri ya Kongo pia.
Angola ni nchi tajiri kwa mafuta na madini: almasi ndiyo muhimu zaidi. Lakini nchi ni maskini kutokana na vita vya miaka 29; kwanza vita vya kupigania uhuru dhidi ya Ureno iliyofuatwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe hadi mwaka 2002.
Nchi yenyewe hasa ni ya kidemokrasia na inajulikana kama Jamhuri ya Angola (kwa Kireno: República de Angola, kwa matamshi ya IPA: /ʁɛ.'pu.βli.kɐ dɨ ɐ̃.'ɣɔ.lɐ/; kwa lugha za wenyeji: Repubilika ya Ngola).
{{cite web}}
: CS1 maint: date auto-translated (link) (Archived 2023 edition)