Misri

Jamhuri ya Kiarabu ya Misri
Gumhūriyyat Misr al-ʿArabiyya (Kiarabu)
Wimbo wa taifa: Biladi, Biladi, Biladi (Nchi yangu, nchi yangu, nchi yangu)
Mahali pa Misri
Mji mkuuCairo
Mji mkubwaCairo
Lugha rasmiKiarabu
 • Rais
Abdel Fattah el-Sisi
 • Waziri Mkuu
Mostafa Madbouly
Eneo
 • Jumlakm2 1,010,408
 • Msongamano99/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
 • Jumla $2.232 Trilioni [1]
 • Kwa kila mtu $20,799 [1]
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
 • Jumladecrease $380.044 Bilioni [1] (ya 42)
 • Kwa kila mtudecrease $3,542 [1]
HDI (2022) 0.728
Gini (2019)31.9
SarafuPauni ya Misri (EGP)
Msimbo wa simu+20
Jina la kikoa.eg

Misri (kwa Kiarabu: مصر, Masr) rasmi kama Jamhuri ya Kiarabu ya Misri ni nchi iliyoko kaskazini-mashariki mwa Afrika, na sehemu ndogo kwenye Rasi ya Sinai ya Asia. Inapakana na Libya upande wa magharibi, Sudan upande wa kusini, Israeli na Ukanda wa Gaza upande wa kaskazini-mashariki, na upande wa kaskazini na Bahari ya Mediterania. Ikiwa na idadi ya watu wapatao milioni 112, inashika nafasi ya 14 kwa idadi ya watu duniani na ya tatu kwa idadi ya watu barani Afrika. Cairo ndiyo mji mkuu na jiji kubwa zaidi la Misri.

Misri inajulikana kwa ustaarabu wake wa kale, piramidi maarufu, na Mto Nile, mto mrefu zaidi duniani.

  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 "Egypt GDP profile". Iliwekwa mnamo 2025-01-30.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne