Jamhuri ya Rwanda Repubulika y’u Rwanda | |
---|---|
Kaulimbiu: Ubumwe, Umurimo, Gukunda Igihugu (Kinyarwanda: "Umoja, Kazi, Uzalendo") | |
Wimbo wa taifa: Rwanda Nziza | |
Mji mkuu na mkubwa | Kigali |
Lugha rasmi | Kinyarwanda, Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili |
• Rais | Paul Kagame |
Historia | |
• Himaya ya Ujerumani | 1884 |
• Utawala wa Ubelgiji | 1916 |
• Uhuru kutoka Ubelgiji | 1 Julai 1962 |
Eneo | |
• Jumla | km2 26,338 (ya 144) |
• Maji (asilimia) | 6.3% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2024 | 14,368,000 |
• Msongamano | 546/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2024 |
• Jumla | ▲ $45.1 bilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $3,078 |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2024 |
• Jumla | ▲ $14.2 bilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $974 |
HDI (2022) | ▲ 0.534 |
Gini (2016) | 43.7 |
Sarafu | Faranga ya Rwanda (RWF) |
Majira ya saa | UTC+2 (CAT) |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +250 |
Jina la kikoa | .rw |
Rwanda, rasmi kama Jamhuri ya Rwanda, ni nchi isiyo na pwani inayopatikana katika Afrika ya Kati-Mashariki.Inapakana na Uganda kaskazini, Tanzania mashariki, Burundi kusini, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo magharibi. Ina idadi ya watu takriban milioni 14.3, ikiwa ya 72 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Kigali. Rwanda imegawanyika katika mikoa 4 na wilaya 30. Inajulikana kwa mandhari yake ya milima yenye kijani kibichi.