Rwanda, rasmi kama Jamhuri ya Rwanda, ni nchi isiyo na pwani inayopatikana katika Afrika ya Kati-Mashariki.Inapakana na Uganda kaskazini, Tanzania mashariki, Burundi kusini, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo magharibi. Ina idadi ya watu takriban milioni 14.3, ikiwa ya 72 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Kigali. Rwanda imegawanyika katika mikoa 4 na wilaya 30. Inajulikana kwa mandhari yake ya milima yenye kijani kibichi.
- ↑ 1.0 1.1 "World Economic Outlook database: April 2022". imf.org.