Alfabeti

Mifumo ya mwandishi duniani
Alfabeti:  Kilatini ,  Kikirili ,  Kilatini pamoja na Kikirili ,  Kigiriki ,  Kigeorgia na Kiarmenia 
Abjadi:  Kiarabu ,  Kiarabu pamoja na Kilatini ,  Kiebrania pamoja na Kiarabu 
Abugida:  Kihindi ya Kaskazini ,  Kihindi ya Kusini ,  Kiethiopia ,  Kithaana   Mwandiko wa kizalendo wa Kanada ,
Alama kwa neno lote na alama za silabi:  Alama za neno lote ,  Mchanganyiko wa alama za maneno na silabi ,  Mchanganyiko alfabeti na silabi   Mchanganyiko alfabeti na silabi 

Alfabeti ni kiasi cha alama zinazotumiwa kuandika sauti za lugha fulani. Alama hizi hupatikana kama orodha kwa ufuatano uliokubaliwa, kwa mfano katika Kiswahili: "a, b, ch, d, dh, e, f, g, gh, h, i, j, k, kh, l, m, n, ny, ng', o, p, r, s, sh, u, t, th, v,w, y, z".

Jina la "alfabeti" hutokana na mwandiko wa Kigiriki ambamo herufi mbili za kwanza ni α "alfa" na β "beta".

Alfabeti ni mtindo wa mwandiko uliosambaa duniani kote. Kwa lugha nyingi imechukua nafasi ya miandiko ya awali.

Alfabeti huonyesha sauti si maneno kamili - hii ni tofauti na mwandiko kama Kichina wenye alama kwa ajili ya neno lote.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne